LIVE STREAM ADS

Header Ads

Watatu wauawa Jijini Mwanza, wengine wadhaniwa kutoroka na silaha

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Watu watatu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wameuawa na Jeshi la Polisi Mkoa Mwanza katika Mtaa wa Nyakabungo, Kata ya Isamilo Jijini Mwanza, usiku wa kuamkia leo Februari 06, 2019.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Mwanza, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Advera Bulimba amesema miili ya watu hao imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mwanza Sekou Toure kwa ajili ya utambuzi na kwamba katika tukio hilo, inadhaniwa watuhumiwa wengine watatu walifanikiwa kutoroka.
Tazama BMG Online TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.