Sekou Toure yaibuka Hospitali Bora, Mongella ataka watumishi wapewe motisha
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mkuu wa Mkoa
Mwanza, John Mongella (anayeongea) ameutaka uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mwanza
Sekou Toure, kuandaa utaratibu wa kutoa motisha kila mwezi kwa watumishi wa Hospitali
hiyo wanaofanya kazi kwa juhudi zaidi.
Mongella
alitoa rai hiyo jana kwenye kwenye hafla ya Benki ya CRDB kukabidhi hundi ya
shilingi Milioni 20 katika Hospitali hiyo,
ili kusaidia ukarabati wa chumba cha upasuaji katika wodi ya akina mama
hospitalini hapo.
Aidha
aliwapongeza watumishi wa Hospitali ya Sekou Toure kwa juhudi zao zilizosaidia kuibuka
Hospitali Bora nchini kwa mwaka wa pili mfululizo na hivyo kuwahimiza kuendelea
na juhudi hizo.
Tazama BMG Online TV hapa chini
No comments: