LIVE STREAM ADS

Header Ads

Benki ya Diamond Trust (DTB) yamuunga mkono Mbunge wa Nyamagana

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com

Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Benki ya Diamond Trust (DTB) imekabidhi mifuko 100 ya saruji kwa mbunge wa jimbo la Nyamagana, Stanslaus Mabula (CCM), ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za maendeleo katika jimbo hilo.
Akizungumza jana kwenye zoezi la kukabidhi mifuko hiyo, Ezra Shandu ambaye ni Meneja Msaidizi DTB Tawi Kuu la Mwanza, alisema lengo ni kusaidia utatuzi wa changamoto mbalimbali katika sekta ya elimu na afya ikiwemo ujenzi wa madara, vyoo pamoja na wodi za afya.

Akipokea mifuko hiyo ya saruji, mbunge Mabula aliishukru benki ya “DTB” na kubainisha kwamba itasaidia kutatua changamoto ya upungufu wa matundu ya vyoo zaidi ya elfu moja pamoja na vyumba vya madarasa takribani 900 katika jimbo la Nyamagana.
Kutoka kushoto ni Meneja Msaidizi DTB Tawi Kuu la Mwanza, Ezra Shandu, Meneja DTB Tawi Kuu la Mwanza, Nabeel Alnoor, Mbunge jimbo la Nyamagana, Stanslaus Mabula pamoja na Afisa Masoko DTB Tawi Kuu la Mwanza, Boniphace Mwita.
Tazama BMG Online TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.