Mgodi wa Dhahabu Geita kuanza kusaidia matibabu ya majeraha ya Moto
Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa GGM, Brad Cato akizungumza wakati wa hafla ya kuwaaga wagonjwa walioungua moto.
Mkuu wa
Wilaya Geita, Mhe. Josephat Maganga akizungumza na wagonjwa
waliofadhiliwa na mgodi wa dhahabu Geita. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Meneja
anayeshughulikia Jamii na Miundo Mbinu, Manace Ndoroma (kushoto), Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa GGM, Brad Catto (wa pili kulia) pamoja na Meneja
anayeshughulikia Afya, Mazingira, Usalama na Mafunzo Dkt. Kiva Mvungi (wa
kwanza kulia).
Hafla ya kuwaaga wagonjwa waliopata majeraha ya moto kwa ajili ya kwenda kupata matibabu.
Mgodi wa
Dhahabu wa Geita (GGM) umetumia Jumla ya Shilingi milioni 40 kwa ajili ya
kuwagharamia upasuaji wagonjwa 40 walioathirika na ajali za moto katika
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mwanza, Sekou Toure.
Mwandishi Maalum
Akizungumza
mjini Geita kabla ya kuwasafirisha wagonjwa hao wakiwamo watoto, Mwakilishi wa
Mkurugenzi Mtendaji wa GGM, Brad Cato alisema kwa miaka 17 sasa wakishirikiana
na wataalamu wa afya kutoka Australia wa Shirika la Rafiki Surgical Mission
wamekua wakitoa tiba hiyo bila malipo.
Naye Mkuu wa
Wilaya ya Geita, Josephat Maganga alisema Serikali inashirikiana na GGM kupitia
mfuko maalumu wa huduma za kijamii (CSR) katika kutekeleza miradi mbalimbali ya
maendeleo kwa nia ya kutatua changamoto zinazokumba jamii.
“Kupitia
fedha za CSR, changamoto mbalimbali zimeweza kutatuliwa zikiwemo ujenzi wa
zahanati, barabara na pia tiba za wagonjwa”. Alisema.
Pia alisema
tiba ya upasuaji ina gharama kubwa ambayo ni zaidi ya Sh milioni moja hivyo
msaada huo umeokoa maisha ya wananchi wengi ambao kama wasingetibiwa
wangeteseka na maumivu.
Kwa upande
wake, Mganga Mkuu wa GGM, Dk. Kiva Mvungi alisema kwa miaka iliyopita GGM
imekuwa ikisaidia watoto na watu wazima wenye midomo sungura lakini kutokana na
idadi yao kupungua kila mwaka ndipo walipoanzisha huduma ya kuwasaidia
walioathirika na makovu ya kuungua na moto.
“Kampuni
yetu kwa kushirikiana na Serikali tumekuwa tukisaidia wagonjwa kila mwaka na
awamu hii ni wale walioathirika na kuunguzwa na moto kutokana na idadi ya
waathirika wa midomo sungura kupungua”. Alisema.
Pia alisema
tatizo la mdomo sungura hutokea pale mama mjamzito anapokosa madini na
virutubisho mbalimbali mwilini ikiwamo ukosefu wa madini ya “folic acid”.
Mmoja wa
wanufaika wa tiba hiyo, Margareth Damian alisema amekuwa akiishi maisha ya
kunyanyapaliwa katika jamii anayoishi huku wakimbatiza majina mengi ya kumbeza.
Alisema
alipata makovu hayo mwaka 2014 baada ya kulipukiwa na jiko la mafuta ya taa
akiwa Shule ya Sekondari Bariadi.
“Nimekuwa
nikiishi maisha ya huzuni kwa sababu pale ninapoishi nimeshabatizwa majina
mengi yakiwemo sura mbili, nashukuru sana kwa msaada huu nina imani majina hayo
yatakoma”. Alisema huku akitokwa na machozi.
No comments: