LIVE STREAM ADS

Header Ads

Baraza la Wazee wilayani Ilemela lafanya uchaguzi

Wasiliana na BMG kupitia 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com kwa huduma za Habari na Mangazo.


Judith Ferdinand, BMG
Baraza la Wazee wa Wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza limehimizwa kutumia chombo hicho kujadili masuala ya wazee pamoja na kuishauri serikali katika nyanja mbalimbali yakiwemo ya kimaendeleo.

Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Paul Wanga aliyasema hayo jana kwenye uchaguzi wa viongozi  mbalimbali wa baraza hilo na kuongeza kwamba chombo hicho sio cha kisiasa bali kimewekwa kwa ajili ya kuwakutanisha wazee ili  kuzungumza mambo yanayo wahusu sanjari na kuishauri Serikali ili kufikia uchumi wa viwanda.

"Baraza limeanzishwa na Serikali kwa lengo mahususi la kuwakutanisha wazee  pamoja na kujadili masuala yanayowahusu sanjari na kuishauri,  msitumike kisiasa kwani siyo la itikadi ya chama chochote, badala yake tumieni  ushawishi mlionao kuleta maendeleo ya wilaya na taifa kwa ujumla". A alisema Wanga.

Alitumia fursa hiyo kuliomba baraza hilo kuandaa katiba ambayo ndio itakuwa muongozo na nyenzo muhimu yenye malengo mahususi ya kusaidia na kuwasilisha masuala mbalimbali ya wazee.
Naye Mwenyekiti wa baraza hilo, Mohamed Yusuph alisema itikadi ya nchi ni kuonyesha uzalendo na kuwa wamoja hivyo viongozi ngazi ya Wilaya na Kata wanatakiwa kutumikia wazee na kupaza sauti kwa serikali.

Baraza hilo lilifanya uchaguzi wa viongozi mbalimbali ikiwemo ya Mwenyekiti ambapo nafasi hiyo alishinda  Mohamed Yusuph aliyepata kura 17, akifuatiwa na Malingumu Sospeter aliyepata kura 14, Kelege Venance kura saba, Michael Urio akipata tano huku kura moja ikiharibika ambapo jumla ya kura zilizopigwa ni zilikuwa 44.

Makamu Mwenyekiti alichaguliwa Prisca Mwisijo baada ya kupata kura 28 kati ya 44 zilizopigwa dhidi ya Janeth Mussa aliyepata 16, huku Katibu akiwa Ndibayukao Muchunguzi aliyepata kura 19 na Katibu Msaidizi akiwa Jackson Kabote aliyepata kura 12.

Nafasi nyingine ni Mweka Hazina ambapo Daniel Makolele aliibuka na ushindi wa kura 35 kati ya 44 zilizopigwa dhidi ya Hamisi Yona aliyepata tisa, huku Saulo Msumari na Mary Selemani wakishinda nafasi ya uwakilishi wa baraza.

No comments:

Powered by Blogger.